Cesc Fabregas Kurudi Arsenal

Tarehe 7 May 2014 - Cesc Fabregas Kurudi Arsenal

Cesc Fabregas anatarajiwa kurudi kwenye klabu yake ya zamani "Arsenal Fc" hii ni kwa mujibu wa mtandao wa SillySeason.com. 

Klabu ya Barcelona  ambayo msimu huu haija fanya vizuri kwenye ligi ya Hispania ina tarajia kuwauza baadhi ya wachezaji wake kwa ajili ya kuimarisha kikosi chao katika kujiandaa na msimu ujao kwakuwa hawajafanya vizuri msimu huu.


Cesc Fabregas
Cesc Fabregas

kwa maana hiyo wachezaji watano wanatarajiwa kuuzwa na Barcelona, katika wachezaji hao  watano Cesc Fabregas ni mmoja wao. magazeti ya hispania yameandika kuwa kama Cesc Fabregas atauzwa basi yeye angependa kurudi Arsenal.


The Gunners wana nafasi kubwa yakumrudisha Fabregas kutokana na mkataba walio sainiana kipindi anauzwa kuainisha kuwa endapo watamuhitaji basi watamnunua kwa Poundi 25 tu.
Kiasi hiki cha pesa Arsene Wenger hawezi shindwa kukitoa ilikumrudisha Fabregas

kwa maana hiyo washabiki wa Arsenal wajiandae kumwona tena Cesc Fabregas ndani ya uwanja wa Emirates