Diamond speaks it all: Amsahauri Wema Sepetu kupunguza Starehe Zisizo na Faida ili afanye Mambo ya Maendeleo


Wema and Diamond

Diamond speaks it all; Amsahauri Wema Sepetu kupunguza Starehe Zisizo na Faida ili afanye Mambo ya Maendeleo. Hii ikiwa ni majibu ya tuhuma zilizo anzishwa na mashabiki wa wema sepetu walio anzisha kampeni ya #BringBackOurWema wakimtuhumu Diamond Platnumz ambae ni mpenzi wa wema sepetu kuwa chanzo cha mwana dada huyo muigizaji wa Bongo movie kushuka ngazi kwenye tasnia ya filamu na kudai kuwa diamond hampi sapoti yoyote ile kama wema anavyo mpa yeye.

Advertisement




Tuhuma hizi zimemfikia Diamond na yeye bila hiyana ame jibu kupitia mtandao wa Instagram ambako choko choko zote zilipoanzia na kusema kuwa wema ndio tatizo kwakuwa  ameendekeza sana maisha ya anasa na mashoga zake  ndio wanaompoteza.

Hiki ndicho alicho kiandika, and I quote:

“Nafikiri ningewaona kweli mnaakili na Mapenzi ya dhati kwa wasanii  wenu….kama mngemshauri apunguze mashoga wapenda anasa na apunguze  Stareh zisizo na Faida, wenda ingemsaidia Pesa kuzitumia kwenye kufanya kazi na kuleta maendeleo badala ya kuwapa viwanda vya pombe…Mimi kama bwana, wajibu wangu ni kuhakikisha Mpenzi wangu anakula vizuri, anavaa vizuri, analala vizuri, na kumuwezesha mtaji wa kufanyia kazi Waswahili wanasema Mchungaji bora anatakiwa aamue kunywa maji!!!!! Au mnataka nikishampa mtaji niache kufanya na show tena na kuigiza nimuigizie mie???? Nisiende Studio nikae dukani nimuuzie mie???? Ni juhudi zako kwanza!...leo hii mimi Hata ningepewa Mamilioni ya mamilioni kama nisingekuwa na moyo mie mwenyewe kwanza kutaka kujituma na kupenda kufanya kazi yangu nisingefikia hapa nilipo!....Mxieeeeeew! Kama nimekuchagua Lamba ndimu usitapike.”